HEBU
TUZUNGUMZE
AFYA
HEBU
TUZUNGUMZE
ELIMU
HEBU
TUZUNGUMZE
HAKI

Wacha tukomeshe ujauzito wa mapema na usiotarajiwa katika Afrika Mashariki na Kusini

 

 

Fikiria kanda la Afrika Mashariki na Kusini ambapo vijana wote wamewezeshwa na wana maarifa, maelezo, uwakala na msaada ili kuzuia ujauzito wa mapema na usiotarajiwa na kufikia uwezo wao kamili.

 

Sheila Khama

  • Kamishna wa zamani na mganga wa kitamaduni

  • Afrika Kusini

  • Sheila anazungumza kuhusu sera za kibaguzi na athari zao mbaya kwa vijana ambao wanapata EUP, na jinsi wanaweza kuzuiwa kupitia mabadiliko ya sera na kuboresha upatikanaji wa huduma za CSE na SRH.

Ilda Simões

  • Msimamizi wa shule ya zamani

  • Msumbiji

  • Ilda anazungumza kuhusu kuwashirikisha wazazi na jamii katika mchakato wa kufanya uamuzi wa utekelezaji wa sera za CSE na SRH, na jinsi hii inasababisha sera bora na zinazotekelezeka za kuzuia EUP na kuingia upya shuleni.

Caroline Boraya

  • Mwanaharakati wa vijana

  • Kenya

  • Caroline anazungumza kuhusu jinsi vijana wanahitaji mtu ambaye wanaweza kumwamini ili awape maelezo sahihi kuhusu ujauzito na afya ya kijinsia.

Mbulelo Dyasi

  • Kiongozi wa kidini

  • Afrika Kusini

  • Mbuelo anazungumza kuhusu jinsi sera za kibaguzi zinavyokuwa na athari mbaya kwa vijana ambao wanapata EUP, na jamii kwa ujumla.

Peris Karuga

  • Msimamizi wa shule

  • Kenya

  • Peris anazungumza kuhusu jinsi elimu kamili ya ujinsia na mawasiliano wazi yatalinda afya ya wanafunzi, kupunguza viwango vya ujauzito wa mapema, na kuwaweka shuleni.

Rudo Msipa Mhonde

  • Mchanganuzi wa data na mzazi

  • Zimbabwe

  • Rudo anazungumzia kuhusu kuwaonyesha watoto wako kuwa unajali ustawi wao kwa kuzungumza nao juu ya vitu vinavyoathiri afya yao--Ikiwa ni pamoja na ngono.

Phumzile Mabizela

  • Kiongozi wa Kidini

  • Afrika Kusini

  • Phumzile anazungumza juu ya hitaji la maelezo sahihi, pamoja na vizuia-mimba, na jinsi yanavyoweza kuboresha afya na ustawi wa wanawake vijana.

Bafana Khumalo

  • Mwanaharakati na mtetezi wa sera

  • Afrika Kusini

  • Bafana anazungumza kuhusu hitaji la kuwashirikisha wanaume na wavulana kwenye mazungumzo juu ya afya ya kijinsia na uzazi, na kufanya kazi katika sekta zote ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma muhimu inatimika.

Shellsy Baronet

  • Msanii

  • Msumbiji

  • Anazungumzia: Shellsy anazungumza kuhusu kuhamasisha vijana kuchukua udhibiti wa maisha yao ya baadaye kwa kujifunza juu ya ngono salama na machaguo yao ya vizuia-mimba na huduma zingine za SRH.

Longton Jamil Hashim

  • Mshawishi wa mitandao ya kijamii

  • Kenya

  • Jamil anazungumza kuhusu umuhimu wa sera za kuingia upya shuleni kwa wasichana wajawazito na walio na watoto na jinsi wanaweza kufaidi vijana na jamii, ili kusababisha ufukiaji wa juu wa elimu.

Video Coming Soon

Shiriki Kampeni

Kwa habari zaidi juu ya kampeni na anwani hii ya wahusika:
letstalkeup@gmail.com